144. MBELE NINAENDELEA

MBELE NINAENDELEA

1.  Mbele ninaendelea,
ninazidi kutembea.
Maombi uyasikie,
Ee Bwana, unipandishe.

Chorus:
Ee, Bwana, uniinue,
Kwa imani nisimame;
Nipande milima yote,
Ee Bwana,
Unipandishe.

2.  Sina tamani nikae,
Mahali pa shaka, kamwe;
Hapo wengi wanakaa,
Kuendelea naomba.

3.  Nisikae duniani,
asumbuapo Shetani;
Natazamia mbinguni,
nitafika na imani.

4.  Nataka nipandishwe juu,
Zaidi yale mawingu.
Nitaomba nifikishwe,
Ee Bwana unipandishe.

Comments

Popular posts from this blog

140. MAHALI NI PAZURI

141. PANA JITO, LINA MAJI MAZURI